47
Ujumbe Kuhusu Wafilisti
1 Hili ndilo neno la
2 Hili ndilo asemalo
“Tazama jinsi maji yanavyoinuka huko kaskazini,
yatakuwa mafuriko yenye nguvu sana.
Yataifurikia nchi na vitu vyote vilivyomo ndani yake,
miji na wale waishio ndani yake.
Watu watapiga kelele;
wote waishio katika nchi wataomboleza
3 kwa sauti ya kwato za farasi waendao mbio,
kwa sauti ya magari ya adui
na mngurumo wa magurudumu yake.
Baba hawatageuka kuwasaidia watoto wao,
mikono yao italegea.
4 Kwa maana siku imewadia
kuwaangamiza Wafilisti wote
na kuwakatilia mbali walionusurika wote
ambao wangeweza kusaidia Tiro na Sidoni.
mabaki toka pwani za Kaftori.[a]
5 Gaza atanyoa kichwa chake katika kuomboleza,
Ashkeloni atanyamazishwa.
Enyi mabaki kwenye tambarare,
mtajikatakata wenyewe mpaka lini?
6 “Mnalia, ‘Aa, upanga wa Bwana ,
utaendelea mpaka lini ndipo upumzike?
Rudi ndani ya ala yako;
acha na utulie.’
7 Lakini upanga utatuliaje
wakati Bwana ameuamuru,
wakati ameuagiza kuishambulia Ashkeloni