8
Maono Ya Nne: Kikapu Cha Matunda Yaliyoiva
1 Hili ndilo alilonionyesha
Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.”
Ndipo Bwana akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
3
4 Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji,
na kuwaonea maskini wa nchi,
5 mkisema,
“Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita
ili tupate kuuza nafaka,
na Sabato itakwisha lini
ili tuweze kuuza ngano?”
Mkipunguza vipimo,
na kuongeza bei,
na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
6 mkiwanunua maskini kwa fedha,
na wahitaji kwa jozi ya viatu,
na mkiuza hata takataka za ngano
pamoja na ngano.
7
8 “Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili,
nao wote waishio ndani mwake hawataomboleza?
Nchi yote itainuka kama Naili;
itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
9 “Katika siku ile,” asema
“Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia
iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
10 Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo,
na kuimba kwenu kote kuwe kilio.
Nitawafanya ninyi nyote mvae nguo ya gunia
na kunyoa nywele zenu.
Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee,
na mwisho wake kama siku ya uchungu.
11 “Siku zinakuja,” asema Bwana Mwenyezi,
“wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote:
si njaa ya chakula wala kiu ya maji,
lakini njaa ya kusikia maneno ya Bwana .
12 Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari
na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki,
wakitafuta neno la Bwana ,
lakini hawatalipata.
13 “Katika siku ile
“wasichana wazuri na vijana wanaume wenye nguvu
watazimia kwa sababu ya kiu.
14 Wale waapao kwa aibu ya Samaria,
au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’
au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: